Somo La 1 Wito wa Utume kwa Jeremiah

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu
(Yeremia 1)
Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.
Utangulizi: Je, Mungu ana mpango kwa ajili ya maisha yako? Je, matendo ya viongozi na watu wa taifa lako yanaleta tofauti kwa jinsi ambavyo Mungu analitendea taifa lako? Juma hili tunaanza mfululizo mpya wa masomo kuhusu mtu ambaye Mungu alimwita ili kulionya taifa lililomgeuzia Mungu mgongo. Hebu tuchinbue somo letu ili tuone kile tunachoweza kujifunza kuhusu kazi ngumu!


I.      Wito
A.      Soma Yeremia 1:1-3. Chukulia kwamba unasikiliza kisa fulani, na una mashaka kama kinaelezea ukweli. Je, utafanya nini hapo hapo, ili kuwa na uhakika zaidi na kisa hicho? (Unaweza kuulizia kwa undani zaidi. Mtu anayeeleza ukweli atakuwa na habari za kina zaidi.)
1.      Kuna habari gani kuu katika mafungu haya ya mwanzo ya kitabu cha Yeremia? (Habari za kina!)
1.      Mambo gani yanahitimisha unabii wa Yeremia, ule ulioandikwa kwenye hiki kitabu? (Watu wake wanakwenda uhamishoni.)
A.      Soma Yeremia 1:4-5. Mafungu haya yanatoa ushauri gani kuhusu suala la utoaji mimba? (Mungu anatufahamu tangu mwanzo kabisa. Mungu anatupangia majukumu ambayo angependa tuyatekeleze kabla hatujazaliwa. Utoaji mimba unaingilia kati mipango ya Mungu.)
1.      Je, Yeremia ndiye alikuwa chaguo la kwanza la Mungu kwa ajili ya kutekeleza kazi yake? (Naam!)
1.      Jiweke kwenye nafasi ya Yeremia, ingekuwa vigumu kiasi gani kukataa kuitikia wito wa Mungu? (Mungu aliniambia kwamba ana huu mpango mahsusi kwa ajili ya maisha yangu – na nilizaliwa mpango huo ukiwepo akilini. Nawezaje kumkatalia Mungu?)
A.      Soma Yeremia 1:6. Yeremia ana wasiwasi gani? (Kwamba bado ni mdogo sana.)
1.      Ni jambo gani hasa mahsusi kuhusu ujana wake, linaleta tatizo kubwa? (Uwezo wake wa kuzungumza.)
1.      Je, Yeremia anajaribu kumkatalia Mungu? Je, Yeremia anajaribu kusogeza muda mbele? Je, anaamua tu kuwa mnenyekevu?
A.      Soma Yeremia 1:7-8. Suluhisho la Mungu kwa wasiwasi wa Yeremia ni lipi? (Mungu anasema kuwa atamwambia Yeremia mambo ya kusema.)
1.      Tuchukulie kwamba Mungu anakuita ili uwe mtume/nabii na wewe una wasiwasi kwamba si mzungumzaji mzuri. Je, woga wako halisi ni upi? (Kwamba utafadhaishwa. Watu hawatakuchukulia kwamba u mtu mwema.)
a.      Jibu la Mungu kwa wasiwasi huo ni lipi? (Usiogope. Mungu atakuokoa, Yeremia.)
a.      Una wasiwasi kiasi gani katika ushuhudiaji unaotokana na uwezekano wa wewe kufikiria kudhalilishwa?
A.      Soma Yeremia 1:9. Je, jambo hili linatendaje kazi? Endapo tutafungua kinywa cha Yeremia, je, tutaona fungu la maneno limeshindiliwa kinywani mwake? Ikiwa sivyo (na sidhani kama kuna mtu yeyote anatarajia kuyaona maneno), je, Mungu anafanya nini? (Itakumbukwa kwamba Yesu alipotenda miujiza wakati mwingine alizungumza na mara nyingine alimgusa mtu. Nadhani mguso ni kwa manufaa ya mtu anayepokea muujiza. Yeremia anatiwa hamasa kwa mguso na kwamba ana karama ya pekee kutoka kwa Mungu.)
A.      Soma Yeremia 1:10. Ikiwa Mungu angekupatia majukumu haya, je, ungeyaelewaje?
1.      Angalia mpangilio wa majukumu yake. Je, hiyo inaashiria nini? (Atakuwa anabomoa, kuharibu na kuangamiza kabla ya kujenga.
1.      Chukulia mpangilio huu kwa kuulinganisha na kazi yetu ya injili. Kwa ujumla mtazamo wangu huwa ni kujenga juu ya chochote kilichopo. Je, wakati mwingine tunapaswa kubomoa kabla hatujaanza kujenga?
a.      Ikiwa hivyo ndivyo, ni wakati gani tutafahamu kwamba kubomoa ndilo jambo sahihi? (Nitahitaji maelekezo mahsusi kutoka kwa Mungu.)
I.      Kujaribisha Kifaa
A.      Soma Yeremia 1:11. Angalia jambo nililolibainisha hapo awali. Hii ni mara ya pili tunasoma “Neno la Bwana likanijia.” Hiyo inamaanisha nini? Kumbuka mara ya mwisho Mungu “aligusa” kinywa cha Yeremia. Je, Yeremia yupo katika maono? Je, kweli Mungu anamtembelea? Jambo gani limekuwa likiendelea? (Kwa jinsi Yeremia anavyoandika jambo hili anaonekana kuwa kwenye maono.)
1.      Mungu aliposema “nimetia maneno yangu kinywani mwako,” je, alimaanisha kwamba alimpa Yeremia uwezo wa kupokea ndoto? (Nadhani. Pia anamaanisha kuwa atamsaidia Yeremia kuzungumza.)
A.      Soma tena Yeremia 1:11 na uongezee Yeremia 1:12. Unalielewaje jibu la Mungu? Je, Mungu ana wasiwasi kwamba maono yanaweza yasifanye kazi?
1.      Kila ninapotaka kuongea kwa kutumia mikrofoni, mara zote huwa ninaijaribisha. Huwa sipendi kuijaribisha mara baada ya kuanza kuzungumza. Je, Mungu anaujaribu uwezo wa Yeremia kuona maono kama ninavyojaribisha mikrofoni? (Nadhani. Suala lililopo ni kwamba, “Yeremia, angalia jambo hili linawezekana!”)
A.      Angalia tena Yeremia 1:11-12. Pamoja na “kujaribisha kifaa,” je, Mungu anapeleka ujumbe halisi? (Maoni mengi ya waandishi huwa yanabainisha kwamba mti wa mlozi ndio huwa unakuwa wa kwanza kuchanua. Kimsingi huwa unachanua katika majira ya baridi kali (winter). Endapo unaangalia ishara ya kukaribia kwa kipindi cha majira ya kuchipua (spring), basi utauangalia mti wa mlozi.)
1.      Unapata maana gani katika jambo hili? (Mungu anasema kuwa anaanza mchakato wa hukumu kwa watu wake. Mungu anaangalia jambo hili kwa ukaribu sana ili kuangalia maendeleo yake, kama ambavyo mtu anavyouchunguza mti wa mlozi ili kuona jinsi majira yanavyoendelea.)
A.      Soma Yeremia 1:13-14. Mungu anaongezea nini katika mwendelezo wa jaribio la maono ya Yeremia? (Mungu anaongezea mtazamo mwingine pamoja na ufafanuzi. Unaweza kuona mwendelezo wenye mantiki? Kwanza, Mungu anachunguza ili kuona kama Yeremia anaweza kuona picha (maono) ambayo Mungu anayatuma. Pili, Mungu anaelezea maana ya picha hizo.)
1.      Hii inatufundisha nini kuhusu kufanya ushuhudiaji kwa ajili ya Mungu? (Mungu atatusaidia katika kila hatua.)
I.      Onyo
A.      Soma Yeremia 1:15. Hapo awali tulisoma kwamba sufuria lenye maji yatokotayo na mdomo wake “unaelekea” toka upande wa kaskazini, hii ikifanya ionekane kwamba vitu vilivyomo vichemkavyo vinautishia upande wa kusini. Hii inamaanisha nini? (Maafa yatatokea upande wa kaskazini na yatautesa upande wa kusini. Katika Agano la Kale, rejea ya “kaskazini” mara kwa mara huwa inawazungumzia watu wabaya. Hapa inaonekana kuizungumzia Babeli.)
1.      Neno picha linamaanisha kwamba “viti vya enzi” vya wafalme wa falme za kaskazini vitawekwa malangoni mwa Yerusalemu. Unalinganisha mawazo gani na “malango” ya mji wa nyakati hizo? (Hapo ndipo biashara (Mwanzo 23:10-11) na shughuli za serikali zinapofanyikia.)
1.      Ipi basi, ndio iliyo maana ya maono haya? (Wafalme wa Babeli watatawala biashara na serikali ya Yuda.)
A.      Soma Yeremia 1:16. Kwa nini ufalme mwovu (Babeli) utekeleze hukumu ya Mungu kwa watu wa Mungu? (Watu wa Mungu wamemwacha Mungu. Wanafukiza uvumba na kuabudu kazi za mikono yao wenyewe.)
1.      Hebu tuchimbue suala hili zaidi. Hakuna jirani yangu hata mmoja anayeabudu sanamu aliyoitengeneza. Kiini cha dhambi hii ni kipi? (Mungu aliwaumba wanadamu. Wanadamu wanaweza kutengeneza vitu vingi. Kwa nini wanadamu wanaabudu kitu walichokitengeneza tofauti na kumwabudu Mungu aliyewaumba? Unaweza kuona jinsi jambo hili linavyomtukana na kumfedhehesha Mungu? Unaweza kuona jinsi kitendo hiki kilivyo cha kipumbavu na kisicho na mantiki?
a.      Je, Mungu anauadhibu upumbavu? (Kwa kweli huku ni kumkataa Mungu kwa kiburi cha hali ya juu.)
1.      Lengo la kutengeneza sanamu ni lipi? (Yumkini, itayaboresha maisha yako kwa namna fulani. Itakulinda au kukuletea vitu.)
a.      Je, unaziamini fedha ulizozipata kuweza kukulinda na kukuletea vitu?
a.      Je, unawaamini watu wengine kuweza kukulinda au kukupatia vitu?
a.      Je, unaweza kuona jinsi tatizo la msingi lilivyo katika kuabudu sanamu leo, hata kama hatumwoni mtu yeyote akiabudu sanamu halisi?
1.      Je, inaleta mantiki kwako kuwatumia watu waovu kuwaadhibu watu wa Mungu? Je, tatizo halipo kwa watu wa Mungu kwamba wameingia uovuni? Kwa nini kuwazawadia watu ambao tayari ni waovu? (Wakati majengo yenye minara pacha yaliposhambuliwa mjini New York, watu nchini Marekani waliungana kusema, “Mungu ibariki Marekani.” Wazo lililokuwepo ni kwamba Mungu anapaswa kuwa upande wa Wakristo na si Waislam ambao waliangamiza minara hiyo. Lakini, ujumbe kwa Yeremia unatuambia kwamba Mungu hachunguzi tabia za watu ambao anawatumia kuwaangamiza watu wake. Hatuwezi kusema kwamba hatutapata adhabu kwa sababu tu tunadhani kwamba sisi tu wenye haki zaidi kuliko watu wengine.)
A.      Soma Yeremia 1:17-19. Je, ungependa kuwa Yeremia? Je, utabadilishana naye kazi?
A.      Rafiki, mara nyingine Mungu anatuchagua kwa ajili ya kutekeleza kazi ngumu. Je, utamtumaini katika nyakati ngumu?

I.                   Juma Lijalo: Mgogoro (Kutoka Ndani na Nje)

No comments:

Post a Comment