LEO NI SIKU MAALUM YA KUCHANGIA VYOMBO VYA HABARI VYA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO TANZANIA, TOA KWA MOYO UONE BWANA ATAKAVYOFUNGUA MADIRISHA YA MBINGUNI

Waumini wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato nchini Tanzania wametakiwa kujitokeza kwa  wingi  siku ya sabato ya leo Oktoba 24,2015 kuchangia vyombo vya habari  vya kanisa  hilo Morning Star Radio  na Morning Star Television. Mhazini wa Union ya  Kusini Mashariki mwa Tanzania Jack Manongi ameiambia Morning Star Radio kuhusu  muhimu wa vyombo vya habari katika kueneza utume wa kanisa hilo.  Manongi amewashukuru watu mbalimbali wanaojitokeza kuchangia  vyombo hivi vya habari  kwa kutoa fedha zao,kutangaza na kudhamini vipindi mbalimbali katika vituo hivyo vilivyoko jijini Dar es salaam .
Picha/habari na Mtangazaji Maduhu

No comments:

Post a Comment