MOROGORO: MKUTANO WA WANA ATAPE UMEFUNGULIWA JANA JIONI NA KATIBU WA KONFERENSI YA MASHARIKI KATI MWA TANZANIA (ECT) MCHUNGAJI FRANCIS KATENGU

 Mkutano wa wajasiriamali  na wanataaluma waadventista wa Sabato Tanzania (ATAPE) jioni siku ya jana na umefunguliwa na katibu wa Konferensi ya jimbo la mashariki kati mwa Tanzania Mchungaji Francis Katengu ambaye amesisitiza kufanya kila jambo kwa viwango vilivyo bora pia ni muhimu kujitoa kikamilifu kwa kazi ya Mungu kwani ndio wito wetu mkuu tulioitiwa.
Mkutano huu umeanza tarehe 13 utaishia tarehe 15 Octoba, 2016 unaofanyika katika ukumbi wa HIGHLAND YOUTH CENTER  mkoani Morogoro mnenaji mgeni rasmi anatokea nchini Malekani ndugu Sam Alexander ambaye pia amewasili jana jioni. Ombea mkutano huu.

No comments:

Post a Comment