"VIJANA WAMEPOKEA MPANGO WA GTTK (GIVE THEM THE KEY) KWA HALI KUU"- MCHUNGAJI SUMWA

Mkurugenzi wa huduma za Vijana, Mziki na chaplensia kwa konferensi ya mashariki kati mwa Tanzania kwa kanisa la Waadventista wa Sabato Mchungaji Emmanuel Sumwa ameyasema hapo jana Agosti 27, 2016 katika viwanja vya kanisa la Mikocheni, alisema mbali na changamoto zote, vijana walijitoa kwa kazi ya Mungu na makanisa mengine yakitoa ahadi ya kushiriki mpango huu kwenye makanisa yao.
Mpango huu wa kuwapa vijana ufunguo uliotoka ngazi ya GC umefanyika kwa wiki mbili na umeleta matokeo chanya na watu wakimpokea Bwana kwa njia ya ubatizo.
Taarifa za ubatizo kwenye hitimisho la mkutano wa mpango wa GTTK ni kama ifuatavyo;-
1. Mwenge (Kiaraka)- 20
2. Mikocheni - 13
3. Mwambisi- 12
4. Mabwe Pande- 9
5. Mwananyamala- 9
6. Chuo Kikuu- 2

No comments:

Post a Comment