LESONI JUMAPILI AGOSTI 28: KUAMINIWA NA WATU

Baada ya kuwatakia yaliyo mema, kuwaonesha huruma na kuhudumia mahitaji yao, Yesu “aliishinda Imani yao” Kujiamini (confidence) katika lugha ya kilatini, huundwa na maneno con, maana yake ‘Imani’ Katika Biblia maneno mbalimbali yamejaribu kuelezea maana ya karibu ya neno Imani.

Katika lugha ya Kiebrania mzizi mkuu wa neon Imani ni AMN ambao kwakupitia hilo tunapata neon amina. Wazo la msingi ni kwamba ni la uthabiti na mwendelezo wa kutegemea. Inatupatia wazo la kitu madhubuti, imara ambalo mtu mmoja anaweza kusadiki na kuamini. Mara nyingi hutafsiriwa kama “kuamini” katika muktadha wa Imani ya Mungu yenye kuokoa, na kwa namna nyingine humaanisha “kweli”. Katika muktadha wa mifano ya Kristo katika kushinda Imani za watu, maana yake ilikua kwamba kuamsha aina flani ya Imani ambayo inaonekana kutokua na mashaka yoyote na yenye kujidhatiti, ambayo kwa Yesu ilikua ni kwa kupitia kuchangamana, kuhurumia wenye mahitaji na kuwahudumia watu.
Soma mafungu yafuatayo, ambayo yote yana msingi katika mzizi wa neno AMN (Mwanzo 15:6, Hesabu 14:11, Isaya 7:9, Habakuki 2:4). Imetumikaje katika aya hizi ni kwa jinsi gani linafikisha wazo la kujitumainia na imani?
Katika kiyunani cha agano jipya, mzizi wa neno unaotumika kufikisha kwa kiebrania neno AMN (Imani) ni “pistis” neno hili la kigiriki la Imani humaanisha, Imani,tumaini,uhakika kamili kutumainiwa na neno hili la kigiriki la Imani humaanisha, Imani,tumaini,uhakika kamili kutumainiwa. Katika muktadha wa mifano ya Kristo ya kuzishinda Imani za watu mwonekano waweza kuwa ule wa kuamsha uhakika kamili, Imani , na kuamini katika kukabiliana na kwake na kutokuwa na ubinafsi kwa kujichanganya, na kuhurumia na kuwahudumia.

Ni muhimu kutambua kwamba katika maandiko, popote pale dhana hii ya kujiamini hutokana na binadam, kama katika kujiamini au Imani ya mtu ni mara nyingi huwa na maana mbaya (soma Mika 7:5 na Zaburi 118:9). Huwa na matokeo chanya endapo kujiamini huku kunatokana na Mungu, hili hututahadharisha kama wafuasi waYesu, tumeitwa kuishi kufuatana na mfano wake wa kujichanganya, kuhurumia, na kuwahudumia walio wahitaji. Hata hivyo wakati wale tunao wahudumia wanaonesha kututumainia sisi, nilazima tuwaelekeze kwa Yesu na kile alicho kifanya kwaajili yao.
Kama mtu angejiuliza, “je, Imani ya kweli katika Mungu huonekanaje?” ungejibuje swali hili, na kwanini? Leta jibu lako siku ya sabato

No comments:

Post a Comment