TAREHE KAMA YA LEO AMEZALIWA MUIMBAJI, MDAU WA INJILILEO NA MPIGAJI KINANDA MR JOHN YARED, HII NI HISTORIA FUPI YA UIMBAJI WAKE

John Jared
Pongezi za dhati toka kwenye ofisi ya Shua Media ambayo inamiliki blog ya injilileo, na mapema leo tulifanya mazungumzo na Mr John Yared na tulimtaka aseme historia yake fupi na alijibu kwa kusema haya yafuatayo;-
 "Nilianza muziki mwaka 1998 na nilijiunga na kwaya kijijini kwetu, nikiwa darasa la nne na nilipojiunga na sekondari ya Ikizu High School nimeimba kwaya kwa muda wa miaka 3 na kisha nikahamia Chome High School ya upareni, mimi na kaka yangu James tukaanzisha kwaya ya Vijana pale mwaka 2008 ambayo ipo mpaka leo, baada ya kumaliza form 6 February 2011 nilijiunga rasmi na kwaya kubwa ya TM Music, na nimekuwa nikishirikishwa kuimba vikundi mbali mbali na waimbaji binafsi kama Angel Magoti, The Voice, Mabalozi Temeke, Oola wa Kurasini. Kwa sasa ninaimba kwaya ya Temeke na kikundi cha OVB (Oola Vocal Band) "

No comments:

Post a Comment