LESONI JUMATATU AGOSTI 29:ULINGANIFU MAKINI

Kanisa mojawapo la waadventista wasabato katika nchi za Afrika linakua kwa kasi. Nini siri yao? Viongozi wa kanisa walisema kwamba kuna uhusiano mkubwa kati ya ukuaji huu na kutokua ubinafsi na huduma zisizo na masharti za washiriki wa kanisa lile kwa jamii inayo wazunguka na taifa kwa ujumla. Kujiamini kwa kanisa hili kuliko enea nchi nzima kulichukua umakini wa rais wanchi hiyo. Alihudhuria mkutano mkubwa wa hadhara ulioendeshwa na kanisa hilo la waadventista wasabato aliwashukuru washiriki wakanisa lile kila mmoja kwa huduma yake.

Wakati huo huo kama wawakilishi wa Kristo tunapaswa kutembea katika njia nyembamba. Tunahitajika, kama Yesu alivyo fanya, kuishinda Imani na kujiamini kwao. Lakini Imani na rtumaini lao kwetu linapaswa kupelekwa moja kwamoja kwa Kristo. Sisi ni mifereji tu. Wanamwona Kristo kupitia sisi kwa kutokua wabinafsi, kuwa na upendo, wenye kujali, kujinyima kwa manufaa ya watu wengine na wawe wana vutwa kwetu kama siku zote wafanyavyo wanapo tutazama sisi kwa makini, kwasababu sisi sote tu wadhambi, wanaweza wasipendezwe na yale yote wanayo yaona kwetu.

 Hivyo ni lazima sikuzote tuwaelekeze kwa Yesu, katika yeye pekee wanaweza wakaweka tumaini lao pekee. Sisi wengine mapema au baadae twaweza kuwakatisha tamaa.
Soma 1 Wakorintho 3:1-9,1 Wakorintho 5:1.Paulo anashughulikia nini katika kanisa hili?Ni aina gani ya ushuhuda ingeonekana hapa kama watu hawa wangekuwa wamewaalika wengine katika kanisa lao na kuona kile ambacho Paulo alikizungumza?
Kwa hakika hatuwezi kuwa wakamilifu, au kuwa na kanisa kamilifu kabla ya kutafuta kuwahudumia wengine. Na wakati huo huo,tunapaswa kutafuta kuwa watu wa aina Fulani ambao ni waaminifu na wengine waweze kujifunza kupitia sisi. Na tutaweza kufanya hivyo tu kwa kuwa waaminifu na wenye kuwajali wengine kama Yesu alivyofanya.Kwa hakika hapana shaka kwamba ugomvi na mapambano ndani ya kanisa yangetokomea kama washiriki wangelenga juu ya kuihudumia jamii na kuufunua kwao upendo wa Kristo.

Kama baadhi ya wageni wangeanza kuhudhuria kanisani kwako kila mara, wangeona nini na ni aina gani ya ushuhuda ungewapatia?

No comments:

Post a Comment