UBATIZO: MAANA YAKE NA KUSUDIO NI NINI?

        Kwa njia ya ubatizo tunakiri imani yetu katika kifo na ufufuo wa Yesu kristo, na kushuhudia kufia kwetu dhambi na kusudi letu la kuenenda katika upya wa maisha. Hivyo
tunamkubali kristo kuwa Bwana na Mwokozi, tunakuwa watu wake, na tunapokelewa kama
washiriki wa kanisa lake. Ubatizo ni mfano wa muungano wetu na kristo, msamaha wa
dhambi zetu na kupokea kwetu Roho Mtakatifu.
           

No comments:

Post a Comment