SOMO LA LEO JITUNZE NAFSI YAKO

 Oktoba 30
  Jitunze nafsi yako, na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia. 1 Timotheo 4:16.  

 Agizo  hilo lililotolewa kwa Timotheo linapaswa kuzingatiwa katika kila nyumba, na kuwa ndiyo mamlaka ya kufundishia katika kila familia na kila shule....  Lengo  kuu kuliko yote la vijana wetu lisingekuwa kujitahidi sana kupata kitu fulani kipya. Hapakuwa na kitu kama hicho katika fikra na kazi ya Timotheo. Yawapasa kukumbuka kwamba, mikononi mwa yule adui wa mema yote, maarifa peke  yake yanaweza kuwa uwezo wa kuwaangamiza wenyewe. Alikuwa ni yule kiumbe mwenye akili nyingi sana, yule aliyekalia cheo cha juu miongoni mwa halaiki ile ya malaika, ambaye mwishowe aligeuka na kuwa mwasi; na wengi wa wale walio na mafanikio makubwa kiakili  sasa wanatekwa kwa uwezo wake [Shetani]. Vijana wangejiweka wenyewe chini ya mafundisho ya Maandiko Matakatifu, na kuyaweka kila siku katika mawazo na maisha yao kwa matendo. Hapo ndipo watakuwa nazo sifa za tabia zinazowekwa katika daraja la juu kabisa katika majumba yale ya kifalme kule mbinguni. Watajificha wenyewe ndani ya Mungu, na maisha yao yatashuhudia utukufu wake.  ----- YI, Mei 5, 1898.  "Jitunze  nafsi yako, na mafundisho yako." Wewe mwenyewe unahitaji kuangaliwa kwanza. Jitoe kwanza wewe mwenyewe kwa Bwana ili upate kutakaswa kwa ajili ya kazi yake. Kielelezo chako cha utauwa kitakuwa na nguvu kwa ajili ya ile kweli kuliko ufasaha mkuu sana usioambatana na maisha mazuri. Tengeneza taa ya roho yako, na kuijaza mafuta ya Roho. Tafuta kwake Kristo neema, yaani, ufahamu ulio wazi kama ule, ambayo itakuwezesha kufanya kazi kwa mafanikio. Jifunze kwake maana ya kuwashughulikia wale aliotoa uzima wake kwa ajili yao. Mtenda kazi mwenye talanta nyingi anaweza kufanya kazi kidogo tu, isipokuwa kama Kristo  ameumbika ndani yake, tumaini na nguvu ya uzima. ----- 7BC 916.  Utu  uzima ulio mkamilifu na wenye tabia nzuri hauji kwa nasibu. Ni matokeo ya kujenga tabia katika miaka ile ya mwanzo ya ujana, ni kujizoeza [kuitii] sheria ya Mungu nyumbani.  ----- YI, Mei  5, 1898. Mungu  anangoja kuwatia nguvu [kuwavuvia] vijana kwa uweza ule unaotoka juu, ili wale wote wanaosimama chini ya bendera ile ya Yesu Kristo yenye alama ya damu wapate kufanya kazi ile ya kuwaita, kuwaonya, na kuwaongoza watu katika njia zile zilizo salama, na kuikita miguu ya wengi juu ya ule Mwamba wa Kale.  ----- Letter 66, 1894.

No comments:

Post a Comment