JUMA LA UWAKILI LINAENDELEA KATIKA KANISA LA KIMARA SDA IKIWA NI SIKU YA JUMATANO

SOMO: NAMNA YA KUWA MWAMINIFUMUHUBIRI: MWINJILISTI MOFFATI Kuna mambo mengine inatupasa kuomba kwa bidii sana fungu Yeremia 29:11-13. Suala la maombi katika biblia lilikuwa ni la muhimu sana na mashujaa wengi walishinda kwa kuomba kwa bidii sana na tena kwa imani.Mtu ambaye haombi kwa bidii huyo hupata kwashakoo ya kiroho hata mambo yake hayaendi vizuri,hata katika kuimarisha mahusiano yetu na Mungu ni muhimu pia kusoma kwa bidii Mithali 4:13,2 Walawi 7:14-16.Mwinjilisti Moffati ni moja wa Wainjilisti wanaotumiwa na Mungu katika suala la injili,akitokea kanisa la Ushindi Sda Dsm aliweza kuanza Juma hili la Uwakili siku ya Jumapili ya tarehe 4 Octoba,2015 na kukiwa na maombi kwa wahitaji mbalimbali kila siku na hata leo siku ya jumatano ni kwa ajili ya maombi ya kufunga na kuomba.Ili ukubaliwe na Bwana toa sadaka iliyo kamilifu na ili ukubaliwe kwenye ndoa,elimu,uchumba,maisha,mafanikio yoyote (Kutoka 25:1-2) Sadaka inayokubalika na Bwana ni ile unayotoa kwa furaha na moyo wa upendo na wala sio ya kunung'unika na lawama,ukitoa sadaka iliyokamilifu nyumba italindwa na Bwana na weka imani yako kwenye vitendo. Kabla ya kuzaa toa sadaka hata kama pia umepata mtoto mpeleke kwa Bwana na mtolee sadaka ya shukrani.Uaminifu wetu na uwe katika vitendo hasa kuwahurumia maskini Mithali 19:17 lakini pia kinyume cha hayo wale ambao ni masikini tukiwanyima tulichonacho basi Bwana hatatusikia sisi Mithali 21:13.Penda kuwaza chanya katika kazi ya Bwana kwani kazi hii inalipa na ombi la leo lilikuwa ni Bwana afanye moyo wa kutoa sadaka na pia kuweza kutunza sabato.>>SOMA ZAIDI HAPA<<

No comments:

Post a Comment