MKUTANO _Mamia Ya watu wabatizwa na kujiunga na kanisa la mungu

Posted on Aug 23 2014
Zaidi ya watu 150 wamebatizwa na kujiunga na kanisa la Waadventista wa Sabato tarehe 23 Agosti 2014 mjini Moshi. Mkutano huo unaendeshwa na Makamu wa Mwenyekiti wa kanisa la Waadventista wa Sabato ulimwenguni Mchungaji Geoffrey Gabriel Mbwana akishirikiana na Mchungaji Caleb J. Migombo wote wakitokea nchini Marekani. Mkutano huo ni wa siku 21 kuanzia tarehe 16/08 - 06/09/2014 na unafanyika katika viwanja vya mashujaa mjini Moshi. Sambamba na mkutano huo pia kuna huduma mbalimbali zinatolewa zikiwepo huduma za ushauri nasaa, mafundisho ya Ujasiliamali na mafunzo ya Komputa. Kabla ya mahubiri wasikilizaji wanapata muda mzuri wa kusikiliza masomo ya Afya na Kaya na Familia.


Mchungaji Geoffrey Mbwana akihubiri


Hapa akionyesha kielelezo cha Mwana kondoo


Zaidi ya watu mia moja na hamsini wamebatizwa kama unavyowaona wakiwa wamevalia vazi jeupe.

No comments:

Post a Comment