LESONI JUMATANO AGOSTI 31:THAMANI YA MTAJI WA KIJAMII

Makanisa ni makundi yanayojitolea kwa sehemu kubwa, yanayofanya kazi katika bajeti finyu.Mtaji wa kijamii husaidia husaidia makanisa mahaliakuongeza nafasi ya kuyafikia malengo yake muhimu. Utamaduni wa kale katika baadhi ya nchi huwasaidia wakulima wengine kuleta mavuno yao ni mfano wa mtaji wa kijamii. Hii ni kwamba ingawa inatupasa kuangalia kila hali kwa jinsi yake, lakini pale inapowezekana ni busara kufanya hivyo, tunaweza kushirikiana na wengine ilikuyafikia malengo yetu.

Soma Nehemia 2:1-9.Ni nini iliyokuwa matokeo ya matumani kutoka mbinguni aliyokuwa nayo mfalme Artashasta juu ya Nehemia?
Fedha ambazo alikuwa amepungukiwa (Nehemia) aliomba kwa wenye uwezo wakampatia. Bado Bwana yupo tayari kugusa mioyo ya wale wanao miliki maliza zake kwasababu ya kuendeleza njia ya ukweli. Wale wanaomtumikia Bwana katika kazi zake wanapaswa kupokea msaada ambao anawasukuma watu wake kutoa…Wenye kutoa misaada wanaweza wasiwe na Imani kwa Kristo wala kufahamu maneno yake; lakini michango yao isikataliwe kwasababu hiyo. “Ellen G.White, Prophets and Kings, uk.634.

Huvutia kiasi gani kwamba katika jambo hili Mungu aligusa mioyo ya wapagani ili kuendeleza kazi yake.Hili linapaswa kutufundisha jambo la muhimu sana hapa. Kwa viwango vyovyote vile tunavyoweza kufikia ni lazima tuwe tayarin kufanya kazi pamoja na watu wengine,hata wale wasio na Imani yetu au wasio na Imani kabisa, Kama kwa kufanya hivyo tutaiendeleza kazi ya Kristo kusonga mbele Zaidi. Ingawa kwa hakika tunapaswa kuwa makini katika ushirikiano tunaouanzisha na watu wengine. Kwa uangalifu na kwa njia ya maombi mengi tunaweza kuifanya kazi na wengine ambao michango yao yaweza kuisaidia kazi ile tunayo hitaji kuifanya kwa ajili ya ustawi wa jumuiya yote. Mara kadhaa serikali, hata mashirika binafsi na wafanyabiashara binafsi, wanapovutia na kazi zetu za kujali wengine, watatupatia msaada wao, Msaada huu haupaswi kukataliwa moja kwa moja au kukubaliwa moja kwa moja bila kufikiri. Badala yake, utazamwe kwa maombi na misingi ya vipengele tofauti tofauti, na kwa nyenzo mbali mbali na ushauri wa kutosha kabla ya kufanya maamuzi.
Ni njia zipi unazoweza kujenga “mtaji wa kijamii”katika jamii yako ambao waweza kuleta matokeo chanya, bali sio mafanikio yako bali mafanikio kwa wengine?

No comments:

Post a Comment